SOMO LA 1
ZURIA LA WA WAVU
Leo tuangalie namna ya kushona zuria la wavu.
VIFAA
1. Uzi
2. Wavu wa plastic (wa madirisha wa mbu)
3. Sindano
4. Rastic
5. Markerpen/Pensil
UZI: Huu ndio uzi wetu unaotumika unapatikana maduka ya uzi ya jumla na maduka ya kawaida, unauzwa sh 1500 mwembamba na mnene unauzwa sh 3000
WAVU: Ni ndio wavu wetu wa plastik wa MBU wa madirishani.
SINDANO: Na hii ndio sindano yetu tunayotumia kushonea zuria letu. Inapagikana maduka ya uzi wa jumla. Hii sindano ni zile wanazotumia wasusi kukurochi nywele nazan wadada wanazielewa zaidi.
RASTIC ya Ribon: Kama utapenda
utaiweka pembeni ya zuria lako ili kupendezesha, usipoweka pia haina shida. Utapeleka kwa fundi akakupindie au unapinda mwenyewe tu na sindano ya mkono.
Utakatakata uzi wako vipande vipande vidogo vidogo vya cm 5, tumia rula kupima uzi wako ili ukate vizuri.
NAMNA YA USHONAJI.
Andaa Vuria lako la wavu.
Chora ua lako au mchoro wako kwenye wavu wako.
Ili ushone vizuri kiurahisi kwa kufuata ua au mchoro wako ulochora.
Anza kushona kwa kufuata mstari wa mchoro/ua lako.
Anza kushona kwa kufuata mstari wa mchoro/ua lako.
Anza kushona kwa kufuata mstari wa mchoro/ua lako.
ANGALIA VIDEO NAMNA YA KUSHONA ZURIA LAKO LA WAVU
VIDEO ZA WANAFUNZI WANAOJIFUNZA MAFUNZO YETU
BAADA YA KUSHONA ZURIA LAKO LITAKUWA KAMA HIVII
Kama hujaelewa sehemu muulize mwalimu kupitia wasap 0715139472/07421722722.
Kwa ujumla niwapongeze Sana Sana walimu.....haya mazulia tulizoea kuyaona na kufikiri ni vitu vigumu kumbe kupitia nyie kujitoa kwenu vijana wamegundua wanaweza na wamefurahia Kama Mimi mama....maoni yangu kwa baadae tukijipanga tuwatafutie madarasa kwa kiwango Fulani muweze kuwafundisha vijana na akina mama..binafsi nimefurahia kupita maelezo... Dr Mama Africa
JibuFutaAsante sana kwa ushauri. Tunalifanyia kazi hilo
Futa